DK SHEIN KUHUDHURIA BUNGE LEO.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema Rais Dk. Ali Mohammed Shein, ni Rais halali wa Zanzibar na atahudhuria ufunguzi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma leo.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud, mjini hapa jana.
Alitoa kauli hiyo kufuatia msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuhoji uhalali wa Dk. Shein kuingia Bungeni wakati uchaguzi wa Zanzibar haujakamilika na kupatikana Rais wake.
Waziri Aboud alisema uchaguzi wa Zanzibar umefutwa na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar kifungu cha 28(1) Dk. Shein anaendelea kuwa Rais mpaka hapo Rais anayefuata atakapokula kiapo.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema Rais Dk. Ali Mohammed Shein, ni Rais halali wa Zanzibar na atahudhuria ufunguzi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma leo.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud, mjini hapa jana.
Alitoa kauli hiyo kufuatia msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuhoji uhalali wa Dk. Shein kuingia Bungeni wakati uchaguzi wa Zanzibar haujakamilika na kupatikana Rais wake.
Waziri Aboud alisema uchaguzi wa Zanzibar umefutwa na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar kifungu cha 28(1) Dk. Shein anaendelea kuwa Rais mpaka hapo Rais anayefuata atakapokula kiapo.

No comments:
Post a Comment