Sunday, December 28, 2014

Chombezo: MPANGAJI
Sehemu: 14
Mtunzi: Frank Masai
Simu: 0717 738973
ILIPOISHIA...
“Huyu ni mgeni,ni mdogo wake George,katoka Dar. Kafika hapa jana usiku wa saa tatu. Anaitwa Prince”.Mzee yule akanitambulisha kwa wanawe ambao mimi nilishaanza kupiga nao stori kidogo kidogo.
“Karibu Prince”.Nikakaribishwa na mabinti wale kwa wao kupokezana kusema karibu Prince.
“Ehee. Prince. Hawa ni wanangu,huyu mkubwa anaitwa Farida Donyo,huyu anaemfata anaitwa Sheila naye ni Donyo na huyu wa mwisho anaitwa Lilian.
SONGA NAYO HAPA
Sasa kitu nilichoona kama mtego kwangu ni pale kifuani,ha ha haaa,nyie watu dunia hii wamebarikiwa sana kwa maujanja. Alikuwa hajafunga vifungo hadi juu,hivyo alifanya yale matiti yake makubwa yanaonekana vizuri sana. Yalikuwa yamevimba halafu yanang’aa kutokana na ule weupe aliokuwa amebarikiwa na MUNGU.
Nilibaki nimechutama pale nilipokuwa natafuta bandeji,lakini sikuchutama bure,bali nilikuwa namuangalia yeye na uzuri wake aliopewa na muumba.
“Mbona umetulia?”.Aliniuliza huku akiwa ametabasamu.
“Nakuangalia wewe unayeingia nyumba ya watu bila hodi”.Nikamjibu.
“Hamna bwana. Samahani kwa hilo. Vipi umepata bandeji”.Aliniuliza.
“Yap. Ndiyo hii hapa nimeipata”.Nilimjibu baada ya kufungua droo moja ya kabati lile lililobeba TV na kukuta hiyo bandeji.
“Okey. Sasa si unanisaidia kubandika?”.Aliniuliza swali la mtego huku anatoa ile khanga yake na kumbakiza na lile gauni la jinzi.
Teheee. Acheni Adam adanganyike tu! kwa Hawa, wanawake wanavishawishi bwana.
Unajua nini? Lile gauni alilivaa lilikuwa linaishia magotini.Kitendo cha kutoa khanga na kisha kukaa kwenye kochi,kilifanya lile gauni kuvutika kwa juu na kuonesha upaja wake ulionona kama umepakwa mafuta ya kula.
“Nitakubandika tu!Mbona rahisi”.Nilimjibu na kumfuata pale alipo na kuibandika ile bandeji.Wakati nambandika alikuwa natoa visauti fulani sijui ni vya raha au maumivu au uchokozi tu! sababu vilikuwa kama vina nisisimua kamanda. Nilipomuangalia usoni,alikuwa kalegeza macho utadhani ananyonywa pango.
Nilijifikiria kwanza kabla sijafanya maamuzi. Kwanza kabisa,ni siku ya kwanza tu!ndo nimefika,lakini huyu manzi anaanza kuleta ishu zake mazee.
Pili nikaona huyu anataka aniletee kesi kama za wakina Tuse,na zaidi nikaona labda ni kicheche hivyo anakitu anataka anifanyie au labda ni mtego ili nifumaniwe.
Mawazo hayo yalipitishwa kwa haraka na bunge la kichwa changu,na nikaona njia mbadala ni kumuacha kama alivyo,kisha nianze kutafuta marafiki ambao watanipa data za familia ile.
Niliichukua khanga yake na kumfunika maungio yake mazuri na mororo.Kisha kamanda nikatabasamu na kukaa karibu yake ili asihisi vibaya.
“Nikuwekee filamu gani”.Niliongea naye kwa upole ili ajisikie amani ya moyo.
“Hauna ile ya Romeo and Juliet?”.Aliniuliza huku akiwa na aibu kidogo.
“Ile ninayo. Kuna CD nilitoka nazo Dar,ipo hiyo. Si ile ya Leonard Decaprio?”Nilimjibu na kumuuliza ili nipate uhakika...
:: Chombezo linazidikunoga hakikisha haikupiti hata siku moja. Kwa wale wote ambao hutoa lugha chafu hapa uwanjani huwa na wa block kundini watu kama hao hawatufai katika kujifunza kupitia hadithi.
:: Endelea ku LIKE na ku COMMENT chombezo hili kali na lakusisimua.
:: Kwa wale watakaokuwa waki SHARE 100 wa kwanza nitawapa kipaumbele kwa kuwa TAG chombezo hili kila litakapokuwa likitoka litakuwa katika 

Saturday, December 20, 2014

ALICE THE SUPER STAR 23

ALICE THE SUPER STAR 23
NA HUSSEIN O. MOLITO
0718 97 56 59
0765 68 48 70
“vipi kuhusu filamu yetu?” aliuliza Alice huku akimuangalia mpenzi wake ambae alikua anatabasamu wakati huo.
“nimekuruhusu pia iingie sokoni… nahitaji kukutengenezea furaha na kupandisha kiwango cha mapenzi yakiyopungua kwa ujinga wangu.” Aliongea Brayton na kumfanya Alice amkumbatie na kumbusu busu kwa furaha.
“ok.. Fanya mawasiliano nae basi...ili asikose.” aliongea Brayton na kuingia chumbani.
“ok my husband to be.” aliongea Alice kwa sauti ya kudeka.
*************************
Mualiko wa Alice na mpenzi wake ulipokelewa vizuri na Larry. Hakusita kufika nyumbani kwa kina Alice na kuingia ndani. Alikuta kumepambwa vizuri kamavile kulikua na ujio wa mgeni kutokea nje ya nchi au kiongozi fulani wa serekalini.
Walikaa meza moja na kupata chakula hicho cha mchana kilichochafua meza.
“karibu sana Larry. Jisikie upo nyumbani.” aliongea Brayton baada ya kuona kimya kimetawala.
“nimeshakaribia.” alijibu Larry na kuendelea kula huku macho yake yakiwa chini bila kumtazama yeyote.
Baada ya kumaliza kula, Walikaa kwenye sofa na kubadilishana mawazo.
“niseme tu ukweli Larry... Kwenye movie yenu umecheza kwa kiwango kikubwa sana. Yaani sikuamini nilipoambiwa kua ndio movie yako ya kwanza kucheza...hongera sana.” aliongea Brayton na kumshika shika Alice ambaye alikua amekaa karibu naye.
Larry alijifanya haoni kitendo hicho na badala yake alikua bize na tv ili kukwepesha macho yake kuona yaliyokua yakiendelea kwa wawili hao.
“nashukuru... Mimi mwenyewe bado naona nimecheza chini ya kiwango... Nataka movie nyingine nikamue zaidi ya pale.” aliongea Larry huku akiwapa masikio pekee lakini macho yote yalikua kwenye Tv.
“nini malengo yako kwa sasa... Maana unakaribia kuwa star?” aliongea Brayton.
“kwa sasa najiangalia tu ili kujua ni kitu gani kingine ninachoweza kufanya ili nisiporomoke hapa nilipo. Napenda sana jina langu likue pamoja na mafanikio yangu. Kwani jina likitangulia bila fedha,...nitaishi kwa shida. Maana nitakua naigiza maisha wakati kuikwelli sijafikia level hizo.” aliongea Larry na kuwaibia kidogo kuangalia ili wasije wakafikiri kua anawaonea wivu.
Safari hii alimuona Alice amelala kabisa kwenye kifua cha mpenzi wake huku Brayton akizichezea nywele za Alice. Ghafla wivu wa mapenzi kwa Alice ukaja tena na kumfanya atamani kuaga. Ila alipiga moyo konde na kufikiria kua atakua ameonyesha udhaifu.
Alitulia kimya na kuanza luwaangalia bila kuangalia pembeni mpaka Alice alipokutanisha macho yake na Larry, aligundua kua alikua anamuumiza Larry na kuamua kunyayuka.
Baada ya maongezi machache, Larry aliaga na kuondoka zake.
Hakujua kua dhamira ya Alice na mpenzi wake ilikua ni nini katika mualiko wao. Kwani haukuishia kwa furaha upande wake. Badala yake ulimfanya ajisikie ameonewa kwa kulingishiwa mtu anayempenda na kumuona akipetiwa na mtu mwengine.
Wakati anawaza, simu yake iiita na jina la Alice likajitokeza kwenye kioo cha simu yake.
Hakuipokea kwa mara kadhaa, baada ya kona Alice anazidi kupiga simu, ndipo alioamua kuipokea.
“sorry Larry... Najua kwanini hupokei simu yangu kwa yale yote uliyoyashuhudia... Halikua kusudio langu wewe uumie. Ila hata mimi nimekwazika kwa jinsi alivyokua akifanya mpenzi wangu. Ili kulinda tu ukaribu wetu na kumuhakikishia kua hisia zake juu ya mimi na wewe kuwa wapenzi zimuondoke na asifikirie tena hilo swala, ndio maana ukaona kama vile nilikua pamoja nae. Ila kusema ukweli hata mimi nimejisikia vibaya sana ...amini hivyo Larry.” aliongea Alice na kumfanya Larry kuwa msikilizaji tu. Larry alivuta pumzi ndefu na kumjibu.
“sawa... Ila tambua kua mimi sitaweza kuja tena nyumbani kwako kwa mualiko wowote ule. Hivyo mtakapofikiria kunialika tena, sitakuja.” aliongea Larry na kukata simu.
Alice alijua kabisa ni jinsi gani Larry alivyoumia kwa tukio lile. Hakujua dhamira ya Brayton kama kumualika Larry ilikua kwa ajili ya kumuumiza tu.
Zilipita wiki tatu baada ya kubandikwa posters za filamu ya The Memory na tarehe ya uzinduz ilifika. Watu wengi waliokua na kiu na filamu hiyo walihdhuria na wengine wakasubiri DVD zilizoanza kuuzwa kama njugu baada tu ya uzinduzi.
Kila aliyebahatika kuiona filamu hiyo, alikiri uwezo wa Larry japo kua ilikua ndio movie yake ya kwanza.
Kutokana na kampuni ya Alice the super star kujulikana Afrika nzima, movie hiyo haikuishia Tanzania peke yake, ilisambaa afrika nzima na baadhi ya nchi za ng`ambo ambaqzo zilikua zinapenda pia kuangalia filamu za kiswahili.
Jina La Larry lilianza kuwa gumzo midomoni mwa watu. Wengi waliokua wakiijua historia yake ya maisha walibaki wameachama midomo na hawakuamini kua ipo siku Larry angefikia kiwango alichofikia hivi sasa.
Zuwena ambaye kwa sasa ameshaolewa na ana mtoto mmoja, aliiangalia hiyo movie na kuujikuta akicheka chini chini. Kwani alifahamu kabisa kua hiyo story ilikua inalenga kabisa maisha yake na Larry walipokua wakiishi pamoja miaka mitano iliyopita.
“mungu amsaidie atimize malengo yake.”
Aliongea kimoyo moyo Zuwena ili mume wake asije kusikia. Maana walikua wanatazama wote hiyo movie.
Rafiki yake wa gereji alifurahi sana baada ya kuona kazi ya rafiki yake aliyempokea na kuanza kubangaiza wote kwenye ofisi yake ndogo ya spare za magari na baadae kukua na kuwa gereji ndogo iliyokua ikiaminika na wamiliki wengi wa magari.
“dua zangu zinafanya kazi mdogo wangu...sema ukibadilisha namba usinikose kwenye namba yako mpya.” aliongea rafiki yake Larry.
“kwanini nibadiliishe namba rafiki yangu?” Aliuliza Larry huku akicheka.
“wewe hujijui kua umeshakua star. Tena zile ndoto zako za kuwa karibu na Alice zimetimia... Sema lile denda mwishoni mzee umelikamua.” aliongea Rafiki yake kiutani.
“haya bwana... Nikipata muda nitakuja hapo tupige story.” aliongea Larry na kukaa simu baada ya rafiki yake kuitikia.
Waandishi wa habari walimtembelea Larry nyumbani kwake na kumuhoji baada ya kumhoji Alice.
“nimejisikia furaha sana kucheza na star mkubwa kama Alice. Nadhani ndio naweza sema kuwa ndio siri ya mafanikio yangu. Pia ile hadithi ya filamu nzima ni ni based on true story. Ndio maana nilikua kama narudia kuigiza maisha yangu ya nyuma. Ndio maana ikawa rahisi kwangu au kufanya kwa hisia kali kwa sababu maumivu yake bado hayajapoa mpaka sasa.”
Aliongea Larry alipokua akijibu swali la mmoja wa waandishi wa habari baada ya kuulizwa siri ya mafanikio yake ya kufanya vizuri kwenye mvie yake ya kwanza.
“tunakutakia mafanikio mema katika tasnia hii ya filamu na ahsante kwa ushirikiano wako kwetu sisi waandishi wa habari.”
Waliongea waandishi wa habari baada ya kuridhika na mahojiano waliyofanya na Larry.
Baada ya waandishi wa habari kuondoka, simu yake iliingia sms ya Alice.
“mgao umeshatoka... Fedha zako zipo kwenye account yako nimeshakuingizia.”
Sms hiyo ndio iliyomfana ampigie simu.
“kwa hiyo unataka kuniambia kua now naweza kwenda kuangalia kiasi cha fedha kilichoingia?... Au kama vipi si unitajie tu.” aliongea Larry huku akionekana kua mwenye furaha sana.
“nina imani kua utashangaa...ila nimeamua tu kutimiza ahadi. Amini kuwa fedha utakayo iona ni asilimia 40 ya mauzo yote ya movie.” aliongea Alice na kuzidi kumtia hamu Larry ya kwe nda kwenye ATM ili aangalie kiasi cha fedha alichoingiziwa.
“naona nachelewa wangu.. Acha niende.” aliongea Larry.
“ok”
Alijibu Alice na Larry alikata simu. Hakuchelewa,aliwasha gari yake na kwenda kwenye Atm iliyokua karibu na maeneo aliyopo na kingiza kadi yake na kuangalia salio.
“OH MY GOD......MILIONI MIA MOJA HAMSINI...ZOTE ZANGU?”
Alishangaa sana Larry baada ya kuona salio limemsomea milioni 151 kutokana na salio lake alilokua amelihifadhi benk liolikua milioni mmoja hapo awali.
ITAENDELEA

Sehemu ya 11

Sehemu ya 11
RIWAYA: ROMEO & JULIETH
MTUNZI: richard R. MWAMBE
MAHALI: LINDI - NANGUMBU
Simu: (whatsapp) +255 767 152125
email: amatagaimba@gmail.com
twitter: Richard Ric Mwambe
SKYPE: Richard Mwambe

CHAPISHO LA 11
NYAKATI ZA PENZI LA MAIKO NA AMANDA.... endelea
11
Maiko alikuwa akimwangalia sana Amanda, mpaka Amanda alihisi aibu kiasi Fulani.
“Mbona waniangalia hivyo?” Amanda aliuliza
“Aaa naustaajabu uzuri wako, nahisi kama ulipendelewa kuumbwa” Maiko alijibu kwa maneno ya utani.
“Mh! Mzuri ntakuwa mimi?” Amanda aliongeza.
“Ee, mwanaume akikusifu kuwa wewe ni mzuri basi ujue ni mzuri kwelikweli,” akainua kinywaji chake na kupiga funda moja kisha akaitua mezani na kuendelea, “Amanda una mpenzi au mchumba?”
Amanda alionekana kushtushwa kidogo na swali lile, akatabasamu na kuruhusu tena vile vishimo mashavuni mwake, hakujua kama kwa kitendo hicho anamuumiza sana Maiko kwani huo ni ugonjwa wake mkubwa.
“Sina Maiko, vipi kwani?” Amanda alihoji
“Ah, hata kama nilitaka kuwa padri lakini nahisi mabadiliko, sasa nahitaji kuwa na wewe mrembo kama hutojali” Maiko alitupa karata yake kwa mtindo huo. Amanda alitulia kimya akiangalia chini huku akichezesha mguu wake wa kushoto ka kuutembezambeza sakafuni, Maiko alikuwa bado ametulia akisubiri nini kitatoka kinywani mwa Amanda. Amanda alinyanyua uso wake na kumtazama Maiko.
“Ninyi wanaume ni waongo sana” Amanda alianza kwa lawama
“Hapana, si wote, ni wachache sana waongo, lakini hii inapelekea kuwa hivi kutokana na ninui wenyewe kuukubali uongo kuliko ukweli” baada ya Maiko kusema hivo wote waliangua kicheko na kugonga viganja vya mikono yao.
“Sina mpenzi wala mchumba, unasemaje?” Amanda aliuliza.
Amanda alimtazama Maiko kwa jicho tata lililomfanya Maiko ajikute anashindwa kumtazama Amanda na kupeleka macho yake pembeni kabisa.
* * *
Penzi changa liliamka kwa Maiko na Amanda, Maiko alimpenda sana Amanda na Amanda vivyo hivyo. Zawadi za hapa na pale zilikuwa si haba kwa wawili hao. Wapo waliomsifu Maiko kwa kupata msichana mrembo kama huyo, na wapo waliomuonea wivu.
Maiko alimtambulisha Amanda nyumbani kwao, wazazi wa Maiko na ndugu zake walimpenda Amanda na kumsifia kwa mengi, daima Amanda alikuwa huru kwenda kwa kina Maiko muda wowote na alipokelewa kwa mikono miwili na familia ya Maiko, naye alijisikia furaha sana kwa hilo, alijisikia nyumbani, mara nyingi alipokwenda alibeba japo zawadi kidogo kwa ajili ya wazazi wa Maiko, wazaa chema.
Ilikuwa ni mazoea yaliyojengeka hata wazazi wa maiko waliweka tick kwenye uhusiano huo na kumsifu kijana wao kuwa anajua kuchagua.
Upande wa pili wa shilingi…
Amanda aliwashirikisha wazazi wake juu ya uhusiano wake na Maiko, haikuingia kichwani kwa baba wa Amanda kwani alionekana wazi kuwa ni jinsi gain alikuwa amechukia kupokea habari hiyo ambayo kwake tuingeiita mbaya, alimtazama binti yake kwa jicho kali sana,
“Nahisi umeanza kurukwa na akili eti?” baba wa Amanda aliuliza, “Sisi wazazi wako ndiyo tunaojua mchumba mzuri anaekufaa wewe, sio we kujichagulia tu huko na huko halafu utuletee mabalaa,”
Amanda alibaki kimya hakujibu neno.
“Lakini baba, mi ndiye nimempenda,” Amanda alisisitiza, kitendo kilichozidi kumchefua baba yake.
“Narudia tena, sisi wazazi wako ndiyo tunaojua mchumba wako ni nani!, usitupangie wewe,” baada ya kusema hayo baba wa Amanda alinyanyuka na kumuwacha Amanda akilia huku mama yake akijaribu kumbembeleza.
Amanda aliumia sana kwa kitendo cha baba yake kumkatalia katakata swala la yeye kuwa na mahusiano na Maiko kwa kigezo kuwa wao kama wazazi wanajua nani wa kuwa mchumba wake, baba wa Amanda bado alikuwa kashika mila za kumchagulia binti mchumba, mila za kizamani, mila zilizosababisha wasichana wengi kuishi kwa taabu katika ndoa zao, kuolewa na watu wasio mioyoni mwao. Mama wa Amanda alimbembeleza sana Amanda na kumuahidi kuwa ataliongea hilo swala na baba yake ili walimalize, hapo Amanda aliona ahuweni kidogo.
Amanda alimpenda sana Maiko, Maiko alikuwa kila kitu kwake, mapenzi motomoto yalikuwa kati wawili hao, ilikuwa ngumu sana kukaa siku mbili bila kuonana, kitendo cha baba wa Amanda kilianza kumpa wakati mgumu Amanda, kilimharibia kesho yake.
* * *
Amanda na Maiko walikuwa wameketi katika moja ya grosari zilizopo katika barabara ya Shauri moyo pembezoni kabisa mwa ukuta wa shule ya Al-Haramain wakiwa na kinywaji baridi katikati yao. Maiko alionekana kuwa mtu mwenye mawazo mengi sana wakati Amanda yeye alionekana katika hali ya kutojielewa. Maiko akamwangalia Amanda, kwa upole akamuuliza
“Kwa hiyo, mipango yetu yote inakufa?”
“Mimi sijui nifanyeje my love, nakupenda Maiko nakupenda sana lakini baba hataki kabisa” Amanda alijibu huku chozi likimdondoka.
Maiko alimshika Amanda mikono yake na viganja vyao vikawa pamoja,
“Amanda, unanipenda kweli?” akamuuliza
“Nakupenda Maiko, sijawahi kupenda namna hii” Amanda alijibu
“Nami nakupenda pia, na sipendi kukupoteza maishani, wewe ni msichana wa maisha yangu, hakuna atakayetutenganisha, au we unasemaje?” maiko aliuliza
“Napenda iwe hivyo, lakini je itawezekana?” Amanda aliuliza.
“Kwa nini isiwezekane? Kama mimi na wewe tumeamua hakika itawezekana”
Baada ya kuzungumza machache wawili hao waliondoka eneo hilo, ilikuwa tayari imetimu saa moja ya usiku, Maiko alimshawishi Amanda waende hadi anakoishi japo akapaone tu maana tangu waanze uhusiano wao miezi kadhaa nyuma Amanda hakuwahi kufika anapoishi Maiko isipokuwa mara nyingi alifika kwa wazazi wa Maiko. Baada ya mvutano kidogo kwa kuwa Amanda alikuwa akikataa kwenda kwa madai kuwa ni usiku sana, alikubali ila akaomba kukaa nusu saa tu. Haikuwachukua muda mrefu walikuwa tayari wamefika, chumba kimoja kidogo cha Maiko chenye kitanda tu ndani yake,
“Vipi, mbona unaonekana kama waogopa?” Maiko alimuuliza
“Lazima niogope, kuingia kwa chumbani kwa mwanaume hujui hatari yake?” alijibu kwa kuuliza
“Ah, hakuna hatari yoyote wasiwasi wako tu, njoo uketi japo ni kitandani,” Maiko alimkaribisha Amanda kuketi huku akimvuta mkono wake kwa mahaba, Amanda kwa hatua za kivivu alikisogelea kile kitanda na kuketi juu yake.
“Ewaaaaa mke wangu mtarajiwa sasa ameketi kitandani mwangu!” maiko alizungumza kwa utaratibu sana sentensi hiyo iliyomfanya Amanda kucheka.
Jioni hiyo manyunyu ya mvua yalianza kuligonga bati la nyumba aliyopanga Maiko, Amanda alianza kuingiwa na hofu juu ya hali hiyo, alimtyazama maiko na kumwambia
“Maiko, mvua, mi naogopa kuchelewa nyumbani nipeleke tafadhali,”
Maiko alimtazama Amanda na kumuuliza
“Sasa unataka kuniacha peke yangu na hali hii mpenzi?”
Amanda alitulia tuli, baada ya sekunde kadhaa alinyayuka na kuuendea mlango, radi kali iliyotengeneza mwanga mkali angani ilimfanya Amanda kurudi ndani na kujitupa kitandani kwa Maiko huku akipiga kelele, mvua ikaanza kunyesha na upepo mkali kuifuatia. Maiko alimuendea Amanda pale kitandani na kumtazama usoni,
“We vipi?” alimuuliza
“Naogopa radi mimi” alijibu Amanda. Mara umeme ukakatika giza likatawala nchi, Maiko hakuwa na mshumaa, aliichukua taa ya ke ya kichina ya kuchaji na kuiwasha lakini ilitoa mwanga hafifu sana ilikuwa haijachajiwa muda mrefu, sekunde chache ikazimika, giza likakijaza chumba kile, Maiko alihisi Amanda akitetemeka sana, akajilaza kitandani na kumkumbatia, mkono wake wa kushoto ukipita juu ya kiuno cha binti huyo, msisimko mkali ukamuingia Amanda ukizingatia maeneo hayo ndiyo yale yenye mtekenyo mkali mwilini mwake.
Amanda alitulia pale kitandani huku kalala kifudifudi, kimya, mkono wa Maiko ulikuwa ukiendelea kutalii kiuno cha binti huyo, shanga zilizokizunguka zilimpa wakati mgumu Maiko.
Kutoka kiunoni mkono ule ulitambaa kuelekea mgongoni, Amanda alitoa miguno hafifu wakati akiufanyia ukarimu wa utulivu mkono wa Maiko ambao ulikuwa ndani ya blauzi yake. Maiko alshusha pumzi ndefu na kumtekenya Amanda, kitendo kilichomfanya Amanda ashtuke na kujigeuza kuangalia, sasa akawa amelala chali. Giza liliwafanya kutokuonana sawasawa, Amanda aliuchukua mkono wa Maiko na kuuweka kitovuni kwake huku asikika kutoa mihemo ya haraka haraka, Maiko aliendelea na shughuli hiyo huku mvua ikiendelea kunyesha, sasa ilikuwa ni kubwa mno, radi kali ilipiga na kumfanya Amanda amvutia Maiko kitandani kwa woga na wote wakajikuta wamekumbatiana kwa nguvu, huku nyuso zao zikielekeana,
“Nakupenda Amanda,” maiko alitamka
“Nakupenda Maiko,” naye alijibu, kisha midomo yao ikakutana mchezo wa kunyonyana ndimi ukachukua nafasi huku kila mmoja akishika sehemu za mwenza kiufundi na mahaba makubwa.
* * *
Amanda alikurupuka kitandani na kumsukumia maiko upande wa pili, akaanza kuhema kwa nguvu kama mtu aliyekuwa akikimbizwa. Alinyanyuka pale kitandani akiwa kama alivyozaliwa baada ya ule mchezo mtamu aliokuwa akiufanya na Maiko, akaiendea stuli ndogo na kuchukua simu ya Maiko kutazama muda, lo, ilikuwa saa sita kasoro robo usiku, Amanda akajawa na hofu, atamueleza nini baba yake, alikuwa wapi, na nani.
“Maiko, nimekwisha!” alilalama
“Nini Amanda?” maiko aliuliza huku akinyanyuka kitandani naye akiwa katika hali ileile.
“Ni saa sita kasoro usiku sasa Maiko nitarudije nyumbani?” Amanda alieleza.
“Amanda,” Maiko aliita huku akisimama na kumuendea Amanda pale alipokuwa amesimama, “Nini shida beibi?” akamuuliza.
“Saa sita kasoro sasa Maiko,” Amanda alijibu huku akilia.
“Basi nyamaza mpenzi” Maiko alimfuta machozi kwa kiganja chake, “Tazama mvua isiyotaka kukatika, unafikiri utaendaje nyumbani? Hata wazazi wako hawatalaumu kukuona sasa kwa maana wanaona hali halisi ya huko nje” maiko alimfariji Amanda.
“Nikodie Tax baba yangu atalipa,” alimwambia Maiko.
Mapigo ya moyo ya Amanda yalikwenda mbio kwa hofu ya kuchelewa nyumbani. Tax ilifika, Maiko na Amanda waliingia na kuondoka, bado mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha.
“Vipi mbona huongei?” Maiko alianzisha mazungumzo
“Ah! Nawaza hapa huko home itakuwaje leo” Amanda alijibu.
Kutokana na mvua iliwachukua kama lisaa limoja kufika kwa kina Amanda, Amanda alishuka na kuuendea mlango wa mbele wa nyumba yao na kugonga kwa fujo. Mara mlango ulifunguliwa na Amanda alikutana uso kwa uso na baba yake, wakabaki wakitazamana.
Amanda aliingia ndani na baba yake akampisha kisha akaufunga mlango nyuma yake.
“Amanda!” baba aliita, Amanda kwa kusikia sauti hiyo alitamani hata kuanguka maana alikuwa akitetemeka kwa woga, akageuka kumtazama baba yake.
“Pole kwa mvua, nenda kapumzike” alimweleza binti yake. Amanda hakuamini, alijua kuwa sasa ndio kunakucha, aliingia chumbani na kujifungia, jambo la kwanza aliishusha kalenda yake ukutani na kuanza kuhesabu tarehe….
::::BABA WA AMANDA ATAFANYA NINI KWA BINTI YAKE?
:::::KWA NINI AMANDA ANAHESABU TAREHE?
:::::NINI KILIWATENGANISHA MAIKO NA AMANDA KATIKA MAPENZI YAO?

Friday, December 19, 2014

MBEGU NJEMA YA USHINDI YAPANDWA KATIKA KONGAMANO LA MAKANISA YOTE YA KIPENTEKOSTE NCHINI TANZANIA

MBEGU NJEMA YA USHINDI YAPANDWA KATIKA KONGAMANO LA MAKANISA YOTE YA KIPENTEKOSTE NCHINI TANZANIA

MUNGU WA MBINGUNI AJIDHIHIRISHA KATIKA KONGAMANO LA MAKANISA YOTE YA KIPENTEKOSTE LILILOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA SABASABA, UKUMBI WA PTA JIJINI DAR ES SALAAM.

Jumamosi ya Tarehe 15.02.2014 palifanyika jambo la baraka na la kihistoria pale ambapo makanisa ya kipentekoste nchini Tanzania,yalipokutana katika Ukumbi wa PTA, Ndani wa Viwanja vya SabaSaba wakiwa wamekutana kwa pamoja, kwa nia moja,Mitume, Manabii, na Wachungaji

Palikuwa na mkusanyiko mkubwa sana wa watu wa Mungu kutoka makanisa mbalimbali ya kipentekoste kama vile Full Gospel Bible Fellowship, TAG, EAGT, EFATHA, Glory of Christ (T) Church-Ufufuo na Uzima, Mito ya Baraka na Mengine mengi.



Mchungaji Zakarya Kakobe akiingia ukumbini

Mchungaji Zakarya Kakobe, mchungaji kiongozi wa Kanisa la full Gospel bible fellowship.



Mchungaji Josephat Gwajima akiingia ukumbini siku ya Kongamano katika ukumbi wa PTA.
Maelfu ya watu waliokuwepo ukumbini wakimshangilia mchungaji josephat Gwajima

 Mchungaji Kakobe akihubiri

 Mchungaji Zacharya kakobe akimkaribisha na kumtambulisha Mchungaji Josephat
 Mchungaji wa Kanisa la Full gospel  bible fellowship Zakarya kakobe akiwa na Mchungaji kiongozi wa Josphat Gwajima

Ukaribisho wa Furaha   



 Mchungaji Kakobe akiendelea kuhubiri.

 Mchungaji Kakobe akiongoza maombi ya kutuma mafarakano kwenye kambi ya adui yako
 Mchungaji Josephat Gwajima katika Maombi

 Mchungaji kakobe akihitimisha maombi
 Muda wa Mchungaji Gwajima kuhubiri uliwadia









MAELFU YA WATU WA MUNGU WAANZA MAISHA MAPYA KATIKA IBADA YA JUMAPILI NA MCHUNGAJI JOSPHAT GWAJIMA

MAELFU YA WATU WA MUNGU WAANZA MAISHA MAPYA KATIKA IBADA YA JUMAPILI NA MCHUNGAJI JOSPHAT GWAJIMA

Ibada ya Jumapili ya Tarehe 12.01.2014 katika Nyumba ya Ufufuo na Uzima Kawe yawa ya Manufaa makubwa sana kwa Maelfu ya watu waliofika Ibadani, ni Baada ya Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima kutangaza rasmi kuwa ni siku ya, kufanya maombi na watu kujiweka huru dhidi ya matatizo na laana za familia. 



SOMO: MATATIZO YA FAMILIA/UKOO
Na. Mch Josephat Gwajima

1 Mambo ya Nyakati 1:1-54
Ni kitabu cha kushangaza sana kwenye biblia sababu kinaelezea tu Fulani akamzaa Fulani, ni kitabu kilichokuwa inanipa taabu sana kukisoma kwenye biblia sababu majina mengine ni magumu hata kuyatamka, nikawa najiuliza hiki kitabu kinamaanisha nini na kwanini kimeandikwa kwenye biblia, nilikuwa sielewi ni nini mtu unaweza kujifunza kwa kuambiwa huyu akamzaa huyu.

Niliposoma kwenye 2 Timotheo 3:16 nikaona kila andiko lililoandikwa lafaa kwa mafundisho, nikajiuliza sasa haya majina ya watu kwenye hiki kitabu yanatufundisha nini? Nilipokuwa natafakari kitabu cha mambo ya nyakati nikapata shock (mshtuko) baada ya kusoma Mathayo 1:1-17 nikaona kitabu hiki kimeanza kwa kuandikwa hiki ni kitabu cha ukoo wa Bwana yesu, nikajiuliza hee hivi Yesu tena ana ukoo.


Nilipoanza kufuatilia huyu Mungu anataja ukoo tena kwanini, 2 Wakorintho 5:17 hata imekuwa mtu akiwa ndani ya kristo amekuwa kiumbe kipya, sasa haya mambo ya ukoo nini tena, niliposhuka kidogo nikaona haya ndiyo makabila 12 ya Yakobo, nikashangaa zaidi kumbe Mungu anajishughulisha na makabila tena. Hapo ndipo nikaanza kujifunza maisha ya mtu anayoishi leo, kama hauishi maisha yanayo mpendeza Mungu maisha yako yatakuwa sawasawa na kabila au ukoo anaotoka. Nikagundua kumbe kuelezea mambo ya familia hakuna tatizo maana hata Mungu yeye mwenyewe ameelezea sana kwenye biblia.




Nikaanza kufuatilia baadhi ya familia nikaona hata usome vipi huwezi kupata upenyo wa maisha, hata Mungu akikuinua kukupeleka ulaya litatokea jambo Fulani litasababisha urudi tu sababu familia hii hawaruhusiwi kupenya, familia hawaruhusiwi kutajirika, familia hawaruhusiwi kumuriki nyumba, familia hawatakiwi kumiriki magari.


Unaweza kuwa umeokoka, lakini kama hujadili na haya mambo ya familia utaingia mbinguni ukiwa umechoka, umekung’utwa kwelikweli, umeokoka lakini unaishi maisha magumu kweli,  unajiuliza mbona kwenye Mathayo 11:28 imeandikwa njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo nami nitakupumzisha, unashangaa mbona mimi sipumziki, kumbe unatoka ukoo wa taabu wenye kulemewa na mizigo na laana (huo ni ukoo wa kutokupumzika).





Hebu jaribu kuangalia maisha ya baba yako na namna alivyo/anavyo malizia maisha yake, kama hakuna jitihada za ziada na wewe utamalizia maisha vile vile. Yesu alikuja ili tukatae kuwa na maisha kama waliyonayo baba/babu zetu, wewe umemuamini Yesu ili akuondolee yale maisha aliyoishi baba yako. Usiseme ukoo wetu sio ukoo wa viongozi, ukoo wetu hatufanikiwagi, ukoo wetu wanakufaga na umri mdogo, usiseme maneno hayo. Useme mama yangu alimaliza hivi lakini mimi nasimama na Bwana Yesu naamua kwenda beyond average, naamua kwenda mbele Zaidi. Usifuate kawaida wewe ukishakuwa umeokoka hauendi kwa kawaida za binadamu.


Ndio maana tunavoanza kuomba tunasema Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo hapa tunakuwa tunajiungamanisha na utajiri na Baraka zote za Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Kabla ya Ibrahimu kulikuwepo na kina Serugi, Tera na kina Nahori lakini hatuanzii huko maana Serugi alikuwa na matatizo yake, Ibrahimu alitengwa na jamaa zake akaambiwa aende kwenye nchi atakayokabidhiwa. Wokovu ni kutengwa, kutengwa na taratibu za ndugu, jamaa, umasikini na mabalaa ya familia. Hivyo ukishaokoka tu maana umetengwa, hupaswi kuwa kama alivyokuwa mama yako au baba yako au babu yako uende extra mile na pale walipoishia walipokutangulia.
 

Sababu itakayokufanya ukimbie kwa nguvu zote kwenda mahala pengine

Mwanzo 9:18-26

“…Hamu ndiye baba wa kanaani…”, “…Hamu baba wa kanaani akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje…”


Ukisoma hayo maandiko utaona Hamu amefanya kosa na baba yake akamlaani kanaani na kizazi chake, na ukiendelea kusoma biblia utaona hiyo laana inavyozidi fuatilia kizazi cha kanaani. Kumbe hata leo kuna matatizo ambayo mtu unaweza kuwa nayo, sio kwamba yamesababishwa na maisha yako unayoishi leo hapana, bali yamesababishwa na makosa waliyo fanya babu wa ukoo, hiyo laana waliyolaaniwa ndiyo inayoendelea kukutafuna hii leo.


Nuhu akalevuka kutoka katika ulevi wake akamlaani kanaani, kanaani analaaniwa kwa kosa la baba yake, aliyeona uchi wa baba ni Hamu lakini laana ikamuangukia kanaani ambaye ni motto wa Hamu. Hapa tunajifunza kile kilichofanyika na mababu kina sambaa kwenye ukoo na vizazi vyote vijavyo, kama ni laana itasambaa kwenye kizazi chote, kama ni Baraka itasambaa kwenye kwenye vizazi na vizazi.

Hebu tuangalie maisha ya watoto waliozaliwa na kanaani

Mwanzo 10:15-19

Ukisoma hapo utaona kabila za wakaanani zikatawanyika na hata sodoma na gomora ilitokea hapo kwenye ukoo wa kanaani, unajiuliza hawa watu wa sodoma na gomora kwanini wanatenda uovu huu, kumbe ni laana ambayo imeendelea kuwafuatilia, hata kuteketea.

Kutoka 3:17

Mungu anasema atawapandisha watu wake kutoka katika mateso ya misri na kuwaingiza katika nchi ya mkaanani nchi iliyojaa asali na maziwa. Utagundua hapo, hawa wakaanani wananyang’anywa nchi yao na watu wa Mungu.

Kutoka 23:23 atawakatilia mbali wa Yebusi, unajiuliza hawa watu wamekosa nini mpaka wapate mateso yote haya, tunagundua ni lile kosa la Hamu kuona uchi wa baba yake, kosa hawakufanya hawa ukoo wa Kanaani lakini ndio laana inaendelea kuwafuatilia.

Kutoka 33:2 “…Nitawafukuza…” Kumbe kufukuzwa ni dalili ya laana

Kumb 20:17

Lakini uwaangamize kabisa Mhiti, na Mwamori, na Mkaanani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi kama alivyokuamuru Bwana Mungu wako. Utaona hapa laana inawafanya hawa watu waangamizwe kabisa, wengine hata hawajui kulikuwa na Hamu ambaye alitenda kosa, lakini laana inaenda nao, na kamwe haiwaachi. Nawe ndivyo ilivyo kuna laana inakufuatilia ambayo leo lazima tuifanyie kazi.

1 Petro 1:18 “…Mwenendo wenu usiofaa mliupokea kutoka kwa baba zenu…” Kumbe kuna mambo yasiyofaa yanayowapata watu leo yalitoka kwa baba zao.

Mambo yaliyokupata kwenye maisha yasikuzuie kupaa kwenda kwenye kesho yako, yote yaliyokupata yalikuwa ni kukunoa uwe upanga mkali kwa ajili ya kesho yako.

Inawezekana leo una laana sababu ya makosa waliyofanya babu zako, babu yako alitesa wenye haki, babu yako alifanya mauaji akalaaniwa na laana inaendelea kwako hadi leo, leo ujitenge na laana za familia, Ibrahimu alitengwa na jamaa na ndugu zake akatangaziwa Baraka na kizazi chake chote hata kuzaliwa kwa Bwana Yesu.

Tanzania maeneo ambayo Mungu asiye Yehova alipoabudiwa kwa muda mrefu ndio masikini kuliko maeneo yote, hiyo ni kwa sababu ya laana ya kuabudu miungu mingine “Biblia inasema usimuabudu Mungu mwingine ila mimi Zaburi 81:9” laana hiyo inakufanya uwe replaced Mungu anakutoa na kumpa mwingine. Unapomuabudu Mungu mwingine ambaye sio Yesu unashangaa watoto wako wanaanza kuondolewa, watoto wako wanaondolewa ni laana hiyo, wakati mwingine unaamua wewe mwenyewe kuacha wenzako wanamiriki.



Namna nzuri ya kutoka kwenye ukoo ni kutoka kama alivyofanya Ibrahimu akaambiwa toka leo kwa jamaa na ndugu zako nenda mpaka nchi nitakayokuonyesha. Kutoka kwetu leo kwenye familia sio kukataa familia, tunatoka kwa namna ya rohoni, tunajitenga na laana zote za familia, unapofanya hivyo mashetani waliotawala familia yako kwa muda mrefu wanakosa nguvu ya kukufuatilia.

Kila unapokataa kwenye ulimwengu wa roho unavunja kitu, unabomoa kitu, na mashetani waliotumwa kulinda ukoo wanakimbia wanajua huyu mtu katukataa.
 
Leo ukatae na kuhama kwenye ukoo wa laana, ukoo wa umasikini, ukoo wa balaa, uhamie ukoo wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, ukoo wa Bwana Yesu. Jitenge na mikosi yote, umasikini kwa jina la Yesu. Ufanye hivyo kwa kumaanisha, na hakika yake utabadirika, hutakuwa kama ulivyo kwa jina la Yesu.

PESA YAIMBA WIMBO