Friday, November 20, 2015

#‎HABARI‬ MAGUFULI AAGIZA PESA ZA SHEREHE YA WABUNGE ZIKASAIDIE MUHIMBILI

Rais John Pombe Magufuli ameagiza kuwa fedha zilizochangwa kwa ajili ya sherehe iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya wabunge na yeye kualikwa, zipelekwe katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kuhudhuria sherehe hiyo na kupokea taarifa kuwa kiasi cha shilingi milioni 225 kilikuwa kimechangwa na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kibenki kwa ajili ya sherehe hiyo ya uzinduzi wa bunge
Kwa mujibu wa Afisa wa Bunge Bw. Said Yakubu, Rais Magufuli ameagiza katika sherehe hiyo zitumike shilingi milioni 24 pekee na nyingine ziende Muhimbili zikasaidie kununua vitanda ili kupunguza tatizo la wagonjwa kulala chini.
Yakubu amesema kuwa agizo hilo la Rais limetekelezwa.

No comments:

Post a Comment

PESA YAIMBA WIMBO