Sunday, January 31, 2016

Kwa mara ya kwanza katika historia ya uhifadhi nchini majangili wa tembo

Kwa mara ya kwanza katika historia ya uhifadhi nchini majangili wa tembo wametungua chopa ya askari wa doria iliyokuwa ikimilikiwa na mwekezaji wa kitalu cha mwiba holdings katika pori la tengefu la maswa wilayani meatu mkoani simiyu na kusababisha kifo cha rubani wa chopa hiyo huku rubani mwenzie akijeruhiwa vibaya mguuni
Chopa hiyo inasemekana ilitunguliwa majira ya saa kumi na mbili jioni jana na Majangilihao ambao wanaosadikika kutumia silaha nzito za kivita walifanikisha kutekeleza uhalifu huo walipo gundua kuwa chopa hiyo ilikuwa ikiwafuatilia baada ya kubaini mahali walipo na uhalifu waliokuwa wakiutekeleza katika pori hilo,ambapo inripotiwa kwamba pamoja na kutungua chopa hiyo walisha fanikiwa kuuwa tembo watatu.

No comments:

Post a Comment

PESA YAIMBA WIMBO