JINI LA DARAJA LA SALENDA-04
Like: www.facebook.com/safina flm
ILIPOISHIA; “Nimekuelewa, acha nikapumzike nyumbani kwani kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute.”
Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka, Suzana alizidi kuchanganyikiwa juu ya hali ya shoga yake. Alijiuliza ni kitu gani kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amwelezee matatizo ya mpenzi wake.
SASA ENDELEA...
Sharifa akiwa na maumivu makali ya chini ya tumbo, alitembea taratibu kurudi nyumbani. Suzana alipata wazo la kumsindikiza shoga yake ambaye aliamini kabisa alihitaji msaada wake. Alitoka haraka nje na kumkuta akimtafuta dereva wa kampuni ampeleke nyumbani.
“Sharifa acha nikupeleke mimi.”
“Suzana endelea na kazi, acha tu nitafika.”
“Haiwezekani, lazima nikusindikize.”
“Mmh! Sawa.”
Suzana alikimbilia kwenye gari lake na kuligeuza haraka kisha akasimamisha pembeni ya Sharifa na kumfungulia mlango. Sharifa aliingia na kufunga mlango. Alimpeleka kwake kupitia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Ajabu walipokaribia Daraja la Salenda, Suzana alipunguza mwendo na kumfanya Sharifa aliyekuwa amejilaza kukaa kitako.
Wote walijikuta wakitupia macho maeneo ya baharini labda wataona kitu chochote lakini hawakuona kitu walichokikusudia zaidi ya kuwaona watu wakitembea juu ya mchanga baada ya bahari kupwa. Baada ya kila mmoja kuwa na uhakika hakuna kitu, Suzana aligeuza uso wake na kubadili gia ili waendelee na safari yao.
Sharifa alikuwa wa kwanza kushtuka na kupaza sauti yake...
“Suzana umemuona yule mwanamke pale pembeni ya barabara?”
Suzana aligeuza shingo tena kuangalia sehemu aliyooneshwa na rafiki yake, kweli alimuona mwanamke mmoja mrefu aliyekuwa amevalia gauni la rangi nyekundu na mtandio wake mwepesi ulioziacha nywele zake nje. Ajabu wakati huo gari lao lilizimika ghafla.
“Suzana vipi, mbona hivyo?”
“Hata mimi nashangaa gari limezimika ghafla.”
“Makubwa, sasa yule dada ni nani?”
“Hata najua, muone jinsi alivyo mzuri, tena anatuchekea labda anatujua.”
“Mmh! Lakini mbona sielewi, nausikia mwili wote ukinisisimka.”
“Siyo wewe tu, hata mimi nasikia nywele zikinisisimka.”
“Mmh! Inawezekana mtu yule si mzuri?”
“Na kweli Suzana, hebu yaone macho yake! Mbona siyaelewi... Mungu wangu! Ona miale inatoka machoni kwake, Suzana washa gari tuondoke.”
Suzana alijaribu kuwasha gari lake lakini liligoma kuwaka, walijikuta wakizidi kupagawa na kutamani kupiga kelele. Sharifa alishtuka kuona mabadiliko kwa yule mwanamke aliyekuwa bado amesimama sehemu ile ile chini ya mti.
“Suzana haya ni maajabu!”
“Ya nini?”
“Muone yule mwanamke, si alikuwa amevaa gauni jekundu na mtandio?”
Suzana alinyanyua uso kumuangalia yule mwanamke na kumuona akiwa na gauni lingine la rangi pinki lililokuwa limempendeza zaidi ya mwanzo, nywele zake zikiwa zimetengenezwa vizuri na kuongeza urembo wake.
“Mmh! Kweli! Kama sikosei alikuwa na gauni jekundu.”
“Unajua yule si kiumbe wa kawaida, huenda ni jini.”
“Jini?”
Kauli ile ilifanya wasikie msonyo mkali ambao ulifanya tumbo la Sharifa livurugike ghafla, baada ya muda lilitulia na kurudi katika hali ya kawaida. Yule mwanamke waliyekuwa wanamshangaa aliwapungia mkono kama anawafahamu, wakajikuta wote wakimpungia mkono, aligeuka na kuondoka kuelekea baharini.
Walijikuta wakimsindikiza kwa macho yule mwanamke aliyeanza kuelekea katikati ya bahari na kupotea machoni mwao.
“Mmh! Suzana hii nini?”
“Hata sijui.”
“Sasa yule atakuwa nani?”
“Yaani nazidi kuchanganyikiwa, ulisikia ule msonyo?”
“Nisiusikie vipi wakati umelifanya tumbo langu lingurume na kutulia.”
Ajabu nyingine, Suzana alipojaribu kuwasha gari liliwaka, wakaamua kuendelea na safari yao huku kila mmoja akijiuliza yule mwanamke mzuri aliyevalia gauni lenye mshono mzuri ambao hawakuwahi kuuona.
“Jamani haya ni maajabu, sasa yule mwanamke ni jini?”
“Lakini jini gani anavaa nguo nzuri kama zile tena za gharama?”
“Mmh! Makubwa, hata sielewi eneo hili lina nini. Kuna umuhimu wa kuulizia zaidi kwa watu ili tupate ufumbuzi.”
Suzana aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Sharifa, bahati nzuri walimkuta mama yake ameshafika nyumbani kwake. Hali ya Sharifa ilikuwa tofauti na muda mfupi uliopita akiwa ofisini. Alishangaa kujiona akiwa mzima kabisa, wala hakutembea kwa kupinda mgongo kwa maumivu ya tumbo tena.
Hali ile ilimshangaza hata Suzana kumuona shoga yake yupo katika hali nzuri.
“Sharifa vipi maumivu yamekwisha?”
“Huwezi kuamini sasa hivi sijambo kabisa, siumwi chochote mwilini.”
“Mmh! Mbona mwaka huu wa maajabu, kila dakika kinazuka kitu kipya machoni mwangu.”
“Shoga karibu ndani umsalimie mama uwahi kazini.”
Suzana aliingia ndani kwa Sharifa kumsalimia mama yake. Alipoingia nusura akimbie kwa mshtuko, aliyeambiwa ni mama yake Sharifa alikuwa ni yule mwanamke mrembo waliyemuona maeneo ya Daraja la Salenda.
“Karibu mwanangu.”
“A..a..sante.”
Alishangaa kumuona akitabasamu lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.
“Sharifa huyu ndiye mama yangu.”
Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amtambulishe kuwa ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa, muda ule alivaa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi.
Suzana aliaga na kutaka kuondoka baada ya kushindwa kumuelewa mama. Ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kuelewa alichokiona mbele yake.
Kila dakika imekuwa ikimshangaza Suzana, ni kweli aliyemuona mbele yake ni yule waliyemuona baharini na aligeuka na kuwa mtu mwingine?
Akiwa njiani alijiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya mambo aliyokutana nayo ya kumuona mwanamke mzuri aliyebadilika nguo, pia kutambulishwa tena kuwa ndiye mama yake Sharifa. Alijikuta akijiuliza Sharifa huenda naye ni jini lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sharifa, mtu aliyemfahamu muda mrefu hakuonesha kitu chochote cha kumfanya amdhanie kuwa si mtu wa kawaida.
Alijiuliza ilikuwaje amuone akifanana na mwanamke waliyemuona pembeni mwa Barabara ya Ali Hasani Mwinyi karibu na Daraja la Salenda na baadaye kumuona mtu tofauti. Aliamua kurudi ofisini kuendelea na kazi.
******
Jioni akiwa nyumbani alipigiwa simu na Sharifa, aliipokea na kuzungumza.
“Vipi shoga za muda?’
“Nzuri tu, vipi unaendeleaje?”
“Huwezi kuamini sijambo kabisa kama siyo mimi niliyekuja ofisini nikitembea kwa shida, kingine kilichonishangaza ni kukatika ghafla kwa damu yangu ya hedhi.”
“Wewee!”
“Yaani Suzy siamini kila dakika kwangu ni miujiza.”
“Mmh! Makubwa.”
“Halafu Suzy eti kuna kitu gani kisicho cha kawaida ulikiona tulipofika nyumbani?”
“Kitu gani?”
“Kisicho cha kawaida ambacho kilikutisha,” swali lile lilimshtua Suzy na kujiuliza kwa nini ameulizwa.
“Kwa nini umeniuliza swali hilo?”
“We nijibu kuna kitu nataka kukuambia.”
“Ni kweli, we umejuaje?”
“Hivi nd’o nimeingia toka kwa mtaalamu mama alinipeleka.”
“He ! Amesemaje?”
“Mmh! Shoga mazito si ya kuyazungumza kwenye simu.”
“Kwa hiyo?”
“Kama unaweza kuja nyumbani njoo, maana hapa nilipo niliyoelekezwa yamenichosha.”
“Mmh! Lazima nije?”
“Basi shoga njoo usikie mambo ya dunia.”
Taarifa zile zilimfanya Suzana ajiandae haraka haraka na kuingia ndani ya gari lake, tayari kwenda kwa Sharifa akiwa na shauku ya kutaka kujua kitu gani kilichomfanya aseme vile. Alimkuta Sharifa akimsubiri kwa hamu.
“Karibu shoga yangu.”
“Asante.”
“Naona ndiyo unatoka kuoga?’
“Wee acha mwili ulikuwa umechoka kila kona, karibu.”
“Asante,” Suzana alijibu huku akikaa kwenye kochi.
“Mh! Shoga lete habari,” Suzana alianzisha mazungumzo.
“Basi shoga baada ya kuondoka nilibakia na mama na kumueleza yote yaliyonitokea hata tukio la kuonana na yule mwanamke leo.”
“Ehe.”
“Mama alinieleza lazima yule atakuwa jini.”
“Ehe.”
“Basi alinichukua na kunipeleka kwa mzee mmoja mtaalam wa majini, tulipofika tulikaribishwa kwenye chumba kilichokuwa na mkeka na nyuma yake kulikuwa shuka nyekundu, pia kulikuwa na picha za kuchora za simba na viumbe visivyoeleweka.”
“Mmh.”
“Basi mganga huyo kijana akachukua kioo kidogo na kunitaka niweke mkono juu yake na kuniuliza matatizo yangu. Baada ya muda akatanitaka nitoe mkono na kunitaka nikitazame kile kioo kwa muda kisha alishusha pumzi.
<p>
“Huwezi kuamini wakati akikitazama kile kioo jasho lilianza kumvuja yule mganga kama kamwagiwa maji, kitu kilichonishtua sana. Baada ya kushusha pumzi alichukua kitambaa na kukifuta na kutuuliza.”
“Mnataka mtatuliwe matatizo yenu au unataka kujua sababu ya yote yaliyotokea?”
“Wewe utakavyoona inafaa,” Mama alijibu.
“Mama si huwa nasikia eti waganga wanajua kila kitu kilichotokea kabla ya kutibu?” Niliuliza.
“Ni kweli tunajua na yote nimeyaona hapa,” mganga alinijibu.
“Sasa si ungeniambia ili nijue natibiwa kitu gani?”
“Hakuna tatizo, kwa hiyo upo tayari kuyasikia yaliyokusibu?”
“Nipo tayari,” nilimjibu.
“Haya vizuri,” Baada ya kusema vile alichukua unga na kuumwaga mbele yake huku akisema maneno kwa sauti ya chini. Baada ya kusema vile alikichukua kioo na kuangalia tena kwa muda wa kama dakika kumi kisha alitugeukia na kusema:
“Kama nitakuwa nasema uongo naomba ukatae, sitaki nionekane nazungumza tofautina ukweli.”
“Sawa.”
“Unaitwa Sharifa, sawa?”
“Ndiyo”
“Umeolewa?”
“Ndiyo.”
“Ndani ya wiki tatu kumetokea matatizo ndani ya ndoa yako?’
“Ndiyo.”
“Wasiwasi wako ni tukio lililokutokea katika Daraja la Salenda?”
“Kweli.”
“Basi ni kweli tatizo lako lilitokana na tukio la darajani ambalo lilipelekea kukuingizia mgogoro ndani ya ndoa yako. Yule uliyekutana naye ni Jini Balikis, kazi yake kubwa ni kuvuruga ndoa za watu. Si wewe tu kuna watu wengi wamekumbwa na mgogoro huu hata kufikia hatua ya kuachana.
“Hata rafiki yako kipenzi ana tatizo hilo, tena yule ndiye chaguo la Jini Balkis kwa vile ni mwanadamu pekee aliyeshuhudia sherehe ya kuagwa kwake kuja duniani.
“ Tuachane na hayo ya shoga yako najua naye ana yake, ila tatizo la mumeo kukosa nguvu za kiume linatokana na kufanya mapenzi na Jini Balkis.
“Kila mnapofanya mapenzi, jini huyo hufika katika eneo la tukio hilo na kuziondoa nguvu za mumeo ili asiweze kukuridhisha vyema.
“Anafanya hivyo makusudi ili aweze kufanya naye mapenzi yeye wakati wa usiku mkiwa mmelala.
“Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri kiasi cha kufikia kukuona wewe hufai tena kwake.”SOMA SEHEMU YA 5 HAPA==>www.2jiachie.com/2014/12/jini-la-daraja-la-salenda-05.html
Kuyajua yote Unatakiwa ku- share simulizi hii SHARE ZINAZIDI Kupungua ndo mwanzo wa kukatisha hii simulizi kuitetea kuendelea kutoka katika page hii baada ya kusoma share hata mara moja Muandishi wa hii simulizi anataka share kuanzia 150na kuendelea vinginevyo itachelewa kutoka......Simulizihii itakujia kila saa nne usiku.
Like: www.facebook.com/safina flm
ILIPOISHIA; “Nimekuelewa, acha nikapumzike nyumbani kwani kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute.”
Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka, Suzana alizidi kuchanganyikiwa juu ya hali ya shoga yake. Alijiuliza ni kitu gani kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amwelezee matatizo ya mpenzi wake.
SASA ENDELEA...
Sharifa akiwa na maumivu makali ya chini ya tumbo, alitembea taratibu kurudi nyumbani. Suzana alipata wazo la kumsindikiza shoga yake ambaye aliamini kabisa alihitaji msaada wake. Alitoka haraka nje na kumkuta akimtafuta dereva wa kampuni ampeleke nyumbani.
“Sharifa acha nikupeleke mimi.”
“Suzana endelea na kazi, acha tu nitafika.”
“Haiwezekani, lazima nikusindikize.”
“Mmh! Sawa.”
Suzana alikimbilia kwenye gari lake na kuligeuza haraka kisha akasimamisha pembeni ya Sharifa na kumfungulia mlango. Sharifa aliingia na kufunga mlango. Alimpeleka kwake kupitia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Ajabu walipokaribia Daraja la Salenda, Suzana alipunguza mwendo na kumfanya Sharifa aliyekuwa amejilaza kukaa kitako.
Wote walijikuta wakitupia macho maeneo ya baharini labda wataona kitu chochote lakini hawakuona kitu walichokikusudia zaidi ya kuwaona watu wakitembea juu ya mchanga baada ya bahari kupwa. Baada ya kila mmoja kuwa na uhakika hakuna kitu, Suzana aligeuza uso wake na kubadili gia ili waendelee na safari yao.
Sharifa alikuwa wa kwanza kushtuka na kupaza sauti yake...
“Suzana umemuona yule mwanamke pale pembeni ya barabara?”
Suzana aligeuza shingo tena kuangalia sehemu aliyooneshwa na rafiki yake, kweli alimuona mwanamke mmoja mrefu aliyekuwa amevalia gauni la rangi nyekundu na mtandio wake mwepesi ulioziacha nywele zake nje. Ajabu wakati huo gari lao lilizimika ghafla.
“Suzana vipi, mbona hivyo?”
“Hata mimi nashangaa gari limezimika ghafla.”
“Makubwa, sasa yule dada ni nani?”
“Hata najua, muone jinsi alivyo mzuri, tena anatuchekea labda anatujua.”
“Mmh! Lakini mbona sielewi, nausikia mwili wote ukinisisimka.”
“Siyo wewe tu, hata mimi nasikia nywele zikinisisimka.”
“Mmh! Inawezekana mtu yule si mzuri?”
“Na kweli Suzana, hebu yaone macho yake! Mbona siyaelewi... Mungu wangu! Ona miale inatoka machoni kwake, Suzana washa gari tuondoke.”
Suzana alijaribu kuwasha gari lake lakini liligoma kuwaka, walijikuta wakizidi kupagawa na kutamani kupiga kelele. Sharifa alishtuka kuona mabadiliko kwa yule mwanamke aliyekuwa bado amesimama sehemu ile ile chini ya mti.
“Suzana haya ni maajabu!”
“Ya nini?”
“Muone yule mwanamke, si alikuwa amevaa gauni jekundu na mtandio?”
Suzana alinyanyua uso kumuangalia yule mwanamke na kumuona akiwa na gauni lingine la rangi pinki lililokuwa limempendeza zaidi ya mwanzo, nywele zake zikiwa zimetengenezwa vizuri na kuongeza urembo wake.
“Mmh! Kweli! Kama sikosei alikuwa na gauni jekundu.”
“Unajua yule si kiumbe wa kawaida, huenda ni jini.”
“Jini?”
Kauli ile ilifanya wasikie msonyo mkali ambao ulifanya tumbo la Sharifa livurugike ghafla, baada ya muda lilitulia na kurudi katika hali ya kawaida. Yule mwanamke waliyekuwa wanamshangaa aliwapungia mkono kama anawafahamu, wakajikuta wote wakimpungia mkono, aligeuka na kuondoka kuelekea baharini.
Walijikuta wakimsindikiza kwa macho yule mwanamke aliyeanza kuelekea katikati ya bahari na kupotea machoni mwao.
“Mmh! Suzana hii nini?”
“Hata sijui.”
“Sasa yule atakuwa nani?”
“Yaani nazidi kuchanganyikiwa, ulisikia ule msonyo?”
“Nisiusikie vipi wakati umelifanya tumbo langu lingurume na kutulia.”
Ajabu nyingine, Suzana alipojaribu kuwasha gari liliwaka, wakaamua kuendelea na safari yao huku kila mmoja akijiuliza yule mwanamke mzuri aliyevalia gauni lenye mshono mzuri ambao hawakuwahi kuuona.
“Jamani haya ni maajabu, sasa yule mwanamke ni jini?”
“Lakini jini gani anavaa nguo nzuri kama zile tena za gharama?”
“Mmh! Makubwa, hata sielewi eneo hili lina nini. Kuna umuhimu wa kuulizia zaidi kwa watu ili tupate ufumbuzi.”
Suzana aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Sharifa, bahati nzuri walimkuta mama yake ameshafika nyumbani kwake. Hali ya Sharifa ilikuwa tofauti na muda mfupi uliopita akiwa ofisini. Alishangaa kujiona akiwa mzima kabisa, wala hakutembea kwa kupinda mgongo kwa maumivu ya tumbo tena.
Hali ile ilimshangaza hata Suzana kumuona shoga yake yupo katika hali nzuri.
“Sharifa vipi maumivu yamekwisha?”
“Huwezi kuamini sasa hivi sijambo kabisa, siumwi chochote mwilini.”
“Mmh! Mbona mwaka huu wa maajabu, kila dakika kinazuka kitu kipya machoni mwangu.”
“Shoga karibu ndani umsalimie mama uwahi kazini.”
Suzana aliingia ndani kwa Sharifa kumsalimia mama yake. Alipoingia nusura akimbie kwa mshtuko, aliyeambiwa ni mama yake Sharifa alikuwa ni yule mwanamke mrembo waliyemuona maeneo ya Daraja la Salenda.
“Karibu mwanangu.”
“A..a..sante.”
Alishangaa kumuona akitabasamu lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.
“Sharifa huyu ndiye mama yangu.”
Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amtambulishe kuwa ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa, muda ule alivaa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi.
Suzana aliaga na kutaka kuondoka baada ya kushindwa kumuelewa mama. Ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kuelewa alichokiona mbele yake.
Kila dakika imekuwa ikimshangaza Suzana, ni kweli aliyemuona mbele yake ni yule waliyemuona baharini na aligeuka na kuwa mtu mwingine?
Akiwa njiani alijiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya mambo aliyokutana nayo ya kumuona mwanamke mzuri aliyebadilika nguo, pia kutambulishwa tena kuwa ndiye mama yake Sharifa. Alijikuta akijiuliza Sharifa huenda naye ni jini lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sharifa, mtu aliyemfahamu muda mrefu hakuonesha kitu chochote cha kumfanya amdhanie kuwa si mtu wa kawaida.
Alijiuliza ilikuwaje amuone akifanana na mwanamke waliyemuona pembeni mwa Barabara ya Ali Hasani Mwinyi karibu na Daraja la Salenda na baadaye kumuona mtu tofauti. Aliamua kurudi ofisini kuendelea na kazi.
******
Jioni akiwa nyumbani alipigiwa simu na Sharifa, aliipokea na kuzungumza.
“Vipi shoga za muda?’
“Nzuri tu, vipi unaendeleaje?”
“Huwezi kuamini sijambo kabisa kama siyo mimi niliyekuja ofisini nikitembea kwa shida, kingine kilichonishangaza ni kukatika ghafla kwa damu yangu ya hedhi.”
“Wewee!”
“Yaani Suzy siamini kila dakika kwangu ni miujiza.”
“Mmh! Makubwa.”
“Halafu Suzy eti kuna kitu gani kisicho cha kawaida ulikiona tulipofika nyumbani?”
“Kitu gani?”
“Kisicho cha kawaida ambacho kilikutisha,” swali lile lilimshtua Suzy na kujiuliza kwa nini ameulizwa.
“Kwa nini umeniuliza swali hilo?”
“We nijibu kuna kitu nataka kukuambia.”
“Ni kweli, we umejuaje?”
“Hivi nd’o nimeingia toka kwa mtaalamu mama alinipeleka.”
“He ! Amesemaje?”
“Mmh! Shoga mazito si ya kuyazungumza kwenye simu.”
“Kwa hiyo?”
“Kama unaweza kuja nyumbani njoo, maana hapa nilipo niliyoelekezwa yamenichosha.”
“Mmh! Lazima nije?”
“Basi shoga njoo usikie mambo ya dunia.”
Taarifa zile zilimfanya Suzana ajiandae haraka haraka na kuingia ndani ya gari lake, tayari kwenda kwa Sharifa akiwa na shauku ya kutaka kujua kitu gani kilichomfanya aseme vile. Alimkuta Sharifa akimsubiri kwa hamu.
“Karibu shoga yangu.”
“Asante.”
“Naona ndiyo unatoka kuoga?’
“Wee acha mwili ulikuwa umechoka kila kona, karibu.”
“Asante,” Suzana alijibu huku akikaa kwenye kochi.
“Mh! Shoga lete habari,” Suzana alianzisha mazungumzo.
“Basi shoga baada ya kuondoka nilibakia na mama na kumueleza yote yaliyonitokea hata tukio la kuonana na yule mwanamke leo.”
“Ehe.”
“Mama alinieleza lazima yule atakuwa jini.”
“Ehe.”
“Basi alinichukua na kunipeleka kwa mzee mmoja mtaalam wa majini, tulipofika tulikaribishwa kwenye chumba kilichokuwa na mkeka na nyuma yake kulikuwa shuka nyekundu, pia kulikuwa na picha za kuchora za simba na viumbe visivyoeleweka.”
“Mmh.”
“Basi mganga huyo kijana akachukua kioo kidogo na kunitaka niweke mkono juu yake na kuniuliza matatizo yangu. Baada ya muda akatanitaka nitoe mkono na kunitaka nikitazame kile kioo kwa muda kisha alishusha pumzi.
<p>
“Huwezi kuamini wakati akikitazama kile kioo jasho lilianza kumvuja yule mganga kama kamwagiwa maji, kitu kilichonishtua sana. Baada ya kushusha pumzi alichukua kitambaa na kukifuta na kutuuliza.”
“Mnataka mtatuliwe matatizo yenu au unataka kujua sababu ya yote yaliyotokea?”
“Wewe utakavyoona inafaa,” Mama alijibu.
“Mama si huwa nasikia eti waganga wanajua kila kitu kilichotokea kabla ya kutibu?” Niliuliza.
“Ni kweli tunajua na yote nimeyaona hapa,” mganga alinijibu.
“Sasa si ungeniambia ili nijue natibiwa kitu gani?”
“Hakuna tatizo, kwa hiyo upo tayari kuyasikia yaliyokusibu?”
“Nipo tayari,” nilimjibu.
“Haya vizuri,” Baada ya kusema vile alichukua unga na kuumwaga mbele yake huku akisema maneno kwa sauti ya chini. Baada ya kusema vile alikichukua kioo na kuangalia tena kwa muda wa kama dakika kumi kisha alitugeukia na kusema:
“Kama nitakuwa nasema uongo naomba ukatae, sitaki nionekane nazungumza tofautina ukweli.”
“Sawa.”
“Unaitwa Sharifa, sawa?”
“Ndiyo”
“Umeolewa?”
“Ndiyo.”
“Ndani ya wiki tatu kumetokea matatizo ndani ya ndoa yako?’
“Ndiyo.”
“Wasiwasi wako ni tukio lililokutokea katika Daraja la Salenda?”
“Kweli.”
“Basi ni kweli tatizo lako lilitokana na tukio la darajani ambalo lilipelekea kukuingizia mgogoro ndani ya ndoa yako. Yule uliyekutana naye ni Jini Balikis, kazi yake kubwa ni kuvuruga ndoa za watu. Si wewe tu kuna watu wengi wamekumbwa na mgogoro huu hata kufikia hatua ya kuachana.
“Hata rafiki yako kipenzi ana tatizo hilo, tena yule ndiye chaguo la Jini Balkis kwa vile ni mwanadamu pekee aliyeshuhudia sherehe ya kuagwa kwake kuja duniani.
“ Tuachane na hayo ya shoga yako najua naye ana yake, ila tatizo la mumeo kukosa nguvu za kiume linatokana na kufanya mapenzi na Jini Balkis.
“Kila mnapofanya mapenzi, jini huyo hufika katika eneo la tukio hilo na kuziondoa nguvu za mumeo ili asiweze kukuridhisha vyema.
“Anafanya hivyo makusudi ili aweze kufanya naye mapenzi yeye wakati wa usiku mkiwa mmelala.
“Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri kiasi cha kufikia kukuona wewe hufai tena kwake.”SOMA SEHEMU YA 5 HAPA==>www.2jiachie.com/2014/12/jini-la-daraja-la-salenda-05.html
Kuyajua yote Unatakiwa ku- share simulizi hii SHARE ZINAZIDI Kupungua ndo mwanzo wa kukatisha hii simulizi kuitetea kuendelea kutoka katika page hii baada ya kusoma share hata mara moja Muandishi wa hii simulizi anataka share kuanzia 150na kuendelea vinginevyo itachelewa kutoka......Simulizihii itakujia kila saa nne usiku.

No comments:
Post a Comment