Monday, December 1, 2014

ANAOMBA USHAURI:

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 21 kwa sasa ninasoma chuo ,katika maisha yangu sijawahi shiriki ngono na mwanaume yoyote yule na nimekuwa mwoga sana kufanya hivyo. Jambo hili limenifanya kuingia katika mahusiano kadhaa na mwisho wa siku wanaume wamekuwa wakinikimbia na kukata mawasiliano na mimi kwakuwa sifanyi ngono. Nimekuwa nikiumizwa sana na hili lakini pia sipo tayari kuupoteza usichana wangu mpaka siku nitakapoolewa. Nimejaribu kuwashirikisha rafiki zangu wa kike wameniambia kama nitaendelea na tabia hiyo, naweza hata nisipate mume maana wanaume wengi wanataka kumjua mwanamke kabla ya kumuoa. Je kuna ukweli katika hilo?Nisaidieni mawazo .

No comments:

Post a Comment

PESA YAIMBA WIMBO