Wednesday, December 3, 2014

ACHA HARAKA, JIFUNZE KUSUBIRI?

ACHA HARAKA, JIFUNZE KUSUBIRI?
Mada yangu leo kama unavyoweza kuiona hapo juu kwenye kichwa chake cha habari, inawazungumzia zaidi akina dada, kwa sababu zilizo wazi kabisa kwamba, wao ndiyo maua ya dunia, bila wenyewe hata maisha sijui yangekuwaje.
Ni jambo la kweli kwamba mara nyingi wanaume ndiyo wanaokuwa wa kwanza kutangaza nia kwa mwanamke tofauti na inavyokuwa kinyume chake. Inapotokea mwanamke ‘anamtokea’ mwanaume, huwa ni gumzo na siyo ajabu kukuta mwanaume akikataa, anaona kama vile anategewa au mwanamke anayemtongoza ana kasoro.
Kwa wanaume, wengi wao hupenda baada ya kukubaliwa katika kutongoza kwao, kinachofuata kiwe ni tendo la ndoa na si vinginevyo wakati kwa wanawake, baada ya kukubaliwa, wao hupenda kwanza wazoeane kwa maongezi, vijizawadi na mitoko ya hapa na pale kabla ya kuhitimisha kwa tendo.
Hii ni hulka ambayo imeendelea hadi kujenga mazoea, kiasi kwamba wanaume wakimpata mwanamke wa kushiriki naye tendo siku ya kwanza tu ya kukutana kwao, huwaona kama wasiofaa. Wamezoea wakikubaliwa, wazungushwe japo siku mbili tatu kabla ya kumalizana.

No comments:

Post a Comment

PESA YAIMBA WIMBO